Kabla ya Harusi unapaswa kuhakikisha kuwa umekaa na
mwenzio na kuelewana juu ya nia yako ya kuamua kufunga ndoa au kufanya Harusi.
Ni jambo jema sana mkiamua kwa pamoja namna, aina na wapi Harusi hiyo
itafanyika, Je Mtaifanyia ukumbini au nyumbani au itaishia tu kanisani au
msikitini?.
Ila ni lazima kuzingatia haya kabla ya
Harusi unayoitarajia!
- Fikiri endapo utafanya sherehe ya Kuvalishwa
au kumvalisha Bi harusi mtarajiwa Pete. " Endapo utaamua kufanya
tendo hilo, Panga siku ya tukio hilo kabisa na mfahamishe mwenza
wako"
- Fikiri kwa pamoja kama je kutakuwa na
Kichen Party au la? Fanya maandalizi yake ili kuhakikisha kuwa
Harusi yenu inafanikiwa.
- Kuna wanaofanya Send Off, Je utafanya hivyo?
Ni Swali la kujiuliza kabla ya Harusi na hili linafanyika kwanza kabla ya
harusi yenyewe.
- Fikiria kama je kutakuwa na tukio maalumu la
kupiga picha maalumu. Andaa location, Kumbuka location au mahali pa
kupigia picha panalipiwa kwa baadhi ya maeneo, hivyo fanya booking mapema
na kama kuna malipo lipia kabisa.
- Fikiria juu ya maandalizi ya Fungate
Mambo Mengine
muhimu yakuzingatia na kufuata kabla na wakati unaandaa harusi yako!
Andaa
File la Kuhifadhi Taarifa za Harusi yako
Ni muhimu sana kuandaa jalada au File ambalo
utalitumia kuweka kumbukumbu za maandalizi ya Harusi yako , ikiwemo Bajeti ya
hausi, Taarifa za vikao, Stakabadhi /Receipts, Majina ya Wageni n.k
Aina ya Harusi
Fikiria kama je unataka harusi ya aina gani, Fikiria unataka harusi ya namna gani, ndogo
au Kubwa , je itahusisha watu wa karibu tu au la, itakuwa
ya kawaida au ya kifahari, ya kati au la?. Endapo utazingatia hili
itakusaidia sana kutimiza swala la Harusi.
Aina ya Ukumbi
Zingatia na Kuwa makini juu ya
hili, Fikiri kwa makini juu ya je waalikwa watasherekea katika ukumbi wa
nje? au wa Ndani? . Na endapo utapata jibu la aina ya ukumbi , nenda
fanya booking, ukiukuta upo wazi lipia malipo tangulizi ili uweze
kujihakikishia kuwa harusi itafanyika kwa siku iliyopangwa.
Usafiri
Fikiria juu ya usafiri wa watu wanaotoka mbali. Hakikishwa
mipango inakamilika kwa wakati?. Fanya Booking ya Hotel au Nyimba
watakayoshukia wageni wako ili kuwahakikishia usalama na malazi katika sehemu
tulivu.
Andaa siku yako ya Harusi
Hakikisha unaandaa siku yako ya harusi kabla ya
kuwashirikisha watu unaotegemea kuwaalika. Kaa na Bi Harusi mtarajiwa mpange
kwa pamoja siku na Mwaka kwa ajili ya Harusi yenu.
Hapa zingatia sana Utayari wa watu wenu wa Karibu
(hasa katika swala la muda), Upatikanaji wa Ukumbi au Kanisa Fulani, Angalia
kama ni siku ya sikukuu au la. Usisahau kuwahusisha familia juu ya hili.
Andaa siku ya kuanza Vikao na
Alika wajumbe katika kikao chako
Hatua hii ni muhimu sana kwani , ni hatua ambayo
inawafanya wajumbe walioalikwa wajisikie wao ni sehemu ya jambo hili na kwamba
wanapaswa kulibeba. Katika vikao vyako hakikisha mambo yafuatayo yanatimizwa:-
·
Bajeti ya Harusi inatengenezwa na kuwasilishwa kwa
wajumbe
·
Mc na
Muziki vinapatikana
·
Watoa huduma zingine wanapatikana ( Pia kupitia
mtandao huu watoa huduma wote utawapata kwa haraka)
·
Ratiba ya
Harusi
·
Kamati
mbalimbali zinaundwa ili kufanikisha Harusi
·
Wajumbe wafahamishwe Rangi ya Harusi
Chagua Wasimamizi
Fikiria juu ya wasimamizi wa harusi yako, Wape taarifa na
uwaeleze namna ya unavyofikiri juu ya harusi yako. Endapo wana mawazo ya
kujenga, wape fursa ya wao kukushauri wanachofikiri ni sahihi.
Mavazi na Mambo mengine yanayoendana
Fikiri
kama unaenda kununu mavazi au unatoa order ya kushonewa, au Unakodisha. Weka
mda wa kutosha juu ya hili ili kupata chaguo la mavazi yaliyo sahihi.
Usiku wa
Harusi
Hakikisha
kuwa unapaki vitu vyako muhimu siku moja kabla ya Harusi. Kwa kufanya hivi itaufanya
usiku wa Harusi yako uende sawia. Kama kuna vitu vinakosekana fanya mpango wa
kununua.
Hakikisha
unaweka vizuri vitambulisho vyako, pass ya kusafiria, au Kadi ya Mpiga kura .
Hii itakusaidia endapo utafika kwenye hotel au sehemu uliyoiandaa kwa ajili ya
kupumzika baada ya harusi na wakahitaji vitu hivyo.
Fungate
Kama
utaenda fungate, fanya maandalizi kabisa, fanya booking ya Hotel au Sehemu
maalumu kwa ajili hiyo,Hakikisha unajiandaa kifedha pia ili kuifanya siku hiyo
kuwa ya kumbukumbu kwenu.
................................................................................................................................................
Karibu Harusi Link | Chang'ombe Mtaa wa Toroli, Dar es Salaam| +255 676 251912/+255 714 992972